Tanzania emblem
Jamhuri ya Muungano wa Tanzania

Tume ya Maboresho ya Kodi

Wasifu

Balozi Ombeni Yohana Sefue
Balozi Ombeni Yohana Sefue
Mwenyekiti

Ni Katibu Mkuu Kiongozi Mstaafu, na Mwanadiplomasia nguli aliyebobea pia katika masuala ya Utawala wa Umma na Sera.

Ana uzoefu wa zaidi ya miaka 47 katika Utumishi wa Umma na amehudumu kama Katibu Mkuu Kiongozi; Balozi na Mwakilishi wa Kudumu katika Umoja wa Mataifa; Balozi nchini Marekani na Mwakilishi Nchini  Mexico; Balozi nchini Canada na Mwakilishi Nchini Cuba; Mwandishi wa Hotuba  na Msaidizi wa Marais wa Awamu ya Pili na ya Tatu.  Kwa miaka mitano (5) alikuwa Mjumbe wa Jopo la Watu Mashuhuri wa Kutathimini Utawala Bora Barani Afrika (APRM), na pia amekuwa Mwenyekiti wa Bodi na Tume mbalimbali.